>
emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania
ega Logo
Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
svg-tree

❓ Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara

Kuna tofuti kubwa kati ya gesi asilia na gesi ya mitungi. Tofauti zake ni kama zifuatazo: -

Gesi asilia ni zao la masalia ya wanyama na mimea vilivyoishi na kuoza na hatimaye kutengeneza mwamba tabaka. Gesi ya mitungi ni mabaki ya mifuta.

GESI ASILIAGESI INAYOHIFADHIWA KWENYE MITUNGI (LPG
Kikemia Gesi asilia ni mchanganyiko wa Gesi mbalimbali kama methane zilizotokea kutokana na kuoza kwa mata ogania kama mimea kwa Miaka mingi iliyopita.LPG ni mchanganyiko wa Hydrocarbon Zaidi ya moja hasa propane na butane na huhifadhiwa katika hali ya kimiminika.
Hupatikana mojamoja toka kwenye miamba ardhini.Hupatikana wakati uzalishaji wa mafuta yanayotumika kwenye magari (Petroli na Dizeli) au wakati wa uzalishaji wa Mafuta na Gesi.

Gesi hii ni nyepesi kuliko hewa na hivyo ina uwezo wa kutawanyika hewani pale inapotokea imevuja na usalama wake ni wa uhakika.

Ni nzito kuliko hewa na pale inapovuja haitawanyiki umbali mrefu.

Husafirishwa/kusambazwa kwa njia ya Mabomba, na kama itasindikwa itasafirishwa kwa meli maalum za LGN (Liquefied Natural Gas) ama CNG (Compressed Natural Gas)Huhifadhiwa katika hali ya kimiminika kwenye matenki au mitungi

 

Kuanzia mwaka 1977 hadi 1999 TPDC ndiyo alikuwa mwagizaji pekee wa bidhaa za petroli nchini. Ilipofika Januari 2000, sekta ndogo ya petroli ilifanywa kuwa huria na kuruhusu makampuni binafsi ya petroli kuagiza bidhaa za petroli na hivyo kuiondoa TPDC katika biashara ya mafuta. Mbali na uingizaji wa mafuta ghafi na bidhaa zake, TPDC pia ilikuwa ikitekeleza majukumu ya udhibiti ikiwa ni pamoja na kupanga bei na kusimamia biashara ya mafuta ya petroli.

Kuanzia mwaka 1977 hadi 1999 TPDC ndiyo alikuwa mwagizaji pekee wa bidhaa za petroli nchini. Ilipofika Januari 2000, sekta ndogo ya petroli ilifanywa kuwa huria na kuruhusu makampuni binafsi ya petroli kuagiza bidhaa za petroli na hivyo kuiondoa TPDC katika biashara ya mafuta. Mbali na uingizaji wa mafuta ghafi na bidhaa zake, TPDC pia ilikuwa ikitekeleza majukumu ya udhibiti ikiwa ni pamoja na kupanga bei na kusimamia biashara ya mafuta ya petroli. Hivi sasa majukumu ya udhibiti yamepelekwa EWURA na uratibu wa uagizaji mafuta unasimamiwa na Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja-PBPA na TPDC imebaki kuwa Kampuni ya Taifa ya Mafuta. Kama mwagizaji pekee, TPDC ilihakikisha usalama wa usambazaji wa bidhaa nchini kote, hii ilihusisha kuhakikisha bidhaa zinapatikana maeneo yote hata maeneo ambayo yalionekana kuwa na mvuto mdogo wa kibiashara kwa makampuni binafsi. Aidha, maeneo yote nchini yalitumia mfumo mmoja wa kupanga bei kupitia uanzishwaji wa mfuko wa kusimamia usafirishaji iliosimamiwa na TPDC. Miongoni mwa mchango wake mkubwa kwa taifa, wakati wa vita vya Tanzania na Uganda (1977-1978) TPDC ilisambaza mafuta ya petroli kwa majeshi ya Tanzania yaliyokuwa mstari wa mbele vitani. Pia, wakati wa mtikisiko wa biashara ya mafuta duniani katika miaka ya 1970 makampuni binafsi yalisita kusambaza mafuta ya petroli kwa hasara lakini TPDC iliokoa hali hiyo kwa kuagiza na kusambaza mafuta pamoja na bidhaa zake nchini.
Mpangilio