Menejimenti ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) imekutana na kufanya Kikao Kazi na Kampuni ya Vitol Group ya nchini Uingereza kwa lengo la kujadili biashara ya kusindika gesi asilia kuwa kimiminika (Liquified Natural Gas).

Kikao kazi hicho kimefanyika ikiwa ni miongoni mwa mikakati ya Serikali kujiandaa katika kutekeleza mradi huo ambapo kwa sasa upo katika hatua za mwisho za majadiliano ya Mkataba wa Nchi Hodhi (HGA).

Kampuni ya Vitol Group ni wabobezi katika biashara ya kuuza na kununua LNG Kimataifa.