Our Latest Blog Posts
18
Jul

TPDC YAUNGA MKONO MPANGO WA NISHATI SAFI NCHINI

‘’Ujenzi wa Kituo mama cha kushindilia gesi asilia kwenye magari (CNG) ni sehemu ya Mpango Mkakati wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuhakikisha Watanzania wote wanatumia nishati safi kwenye magari, kupikia na vyombo vingine vya moto.’’ Hayo yamesemwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati Dkt. James Mataragio wakati alipotembelea eneo la ujenzi wa Mradi wa Kituo MaMa cha…

Read more →
09
Jul

TPDC KUONGEZA KASI YA USAMBAZAJI GESI ASILIA

Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati Mhandisi Felchesmi Mramba amesema Serikali imejipanga kushirikiana na sekta binafsi katika kuongeza kasi ya ujenzi wa miundombinu ya usambazaji wa  gesi asilia majumbani,viwandani  na kwenye magari Akizungumza alipotembelea banda la TPDC kwenye Maonesho ya 48 ya Kimataifa ya Biashara amesema TPDC inaendelea kutekeleza miradi hiyo ya usambazaji gesi asilia katika maeneo mbalimbali hivyo kwa kushirikiana na sekta binafsi itaweza kuwafikia watumiaji wengi zaidi Aidha…

Read more →
01
Jul

DKT.MATARAGIO AKAGUA UJENZI WA KITUO MAMA CHA KUJAZIA GESI ASILIA KWENYE MAGARI

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Dkt. James Mataragio amekagua kazi za ujenzi wa kituo cha kujazia gesi asilia kinachojengwa katika barabara ya Sam Nujoma mkoani Dar es Salaam na kumtaka Mkandarasi kuongeza kasi ya utekelezaji wa mradi kwa kuongeza rasilimali watu na vifaa.Dkt. Mataragio amesema hayo tarehe 01.01.2024 alipofanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa mradi huo. Amesema watanzania wanasubiri mradi husika kwa hamu kubwa hasa katika kipindi…

Read more →
27
Jun

SERIKALI YAONDOA TOZO KWENYE GESI ASILIA

Serikali imeridhia ombi la kuondoa ushuru wa shilingi 382 iliyokuwa imepanga kuweka kwenye kila kilo ya gesi asilia inayotumika kwenye magari kuanzia mwaka ujao wa fedha 2024/25. Ushuru huo umeondolewa kufuatia ushauri wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti ambayo imeeleza kuwa haikubaliani na ushuru huo kwani sekta ya gesi bado ni changa na inaendelea kukua taratibu na hadi sasa haijaweza kutumika kikamilifu nchini kutokana na gharama za kufunga…

Read more →
13
Jun

WAJUMBE WA BODI YA WAKURUGENZI TPDC, WATEMBELEA MIRADI YA UWAJIBIKAJI KWA JAMII (CSR)

Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) limeendelea kuunga mkono juhudi za Serikali katika kuboresha huduma za kijamii kwenye maeneo ambayo shughuli za utafutaji, uzalishaji, usafirishaji na usambazaji wa gesi asilia zinafanyika. Huduma hizo ni pamoja na afya, elimu, maji na utawala bora ambapo huduma hizi ni sehemu ya Uwajibikaji wa Shirika kwa Jamii (CSR). Hayo yamebainishwa katika ziara ya Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya TPDC walipotembelea miradi mbalimbali…

Read more →
12
Jun

TPDC YAPONGEZWA KUENDESHA VIWANDA VYA KUCHAKATA GESI KWA KUTUMIA WAZAWA

Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi TPDC wamepongeza jitihadaa zinazofanywa na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) katika kuwajengea uwezo wafanyakazi wanaoendesha mitambo ya kuchakata gesi asilia Songosongo na Madimba ikiwa ni pamoja na kutoa mafunzo ya muda na muda mrefu ndani na nje ya nchi. Mkakati huu imewezesha wafanyakazi hao kuwa na uwezo mkubwa wa kuendesha mitambo hiyo kwa ufanisi wa hali ya juu. Akiongea baada ya ziara hiyo, Mjumbe…

Read more →
07
Jun

TPDC YAWEKA MKAKATI WA KUWA NA HIFADHI KUBWA YA MAFUTA NCHINI

Hayo yameelezwa katika ziara ya Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) inayoongozwa na Mhe. Balozi Ombeni Sefue wakati wa ziara ya kutembelea miradi ya TPDC iliyopo TIPER Kigamboni leo tarehe 07/6/2024. Lengo la ziara hiyo ni kujionea hali halisi ya miundombonu ya miradi ambayo kwa muda mrefu imekua haitumiki pamoja na kueleza mikakati iliyopo ya ukarabati na ujenzi wa miundimbinu mingine mipya ili nchi iwe…

Read more →
17
May

TPDC, ROSETTA NA AFRICA 50 ZASAINI MKATABA WA UBIA WA KUSAMBAZA GESI ASILIA NCHINI

Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) na Kampuni ya Rosetta ya nchini Misri wamesaini mkataba wa awali wa ubia wa utekelezaji wa mradi wa kusambaza gesi asilia kwa mfumo wa Mini LNG. Mkataba huo umesainiwa leo tarehe 17/05/2024 katika ukumbi wa mikutano wa TPDC ulioko Jengo la Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam. Akizungumza katika hafla hiyo kwa niaba ya Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mkurugenzi Mkuu…

Read more →
02
Apr

NAIBU KATIBU MKUU WIZARA YA NISHATI AFANYA ZIARA TPDC

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Dkt. James Mataragio,amefanya ziara ya kikazi katika  Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) na kuzungumza na Menejimenti ya TPDC  lengo likiwa ni kujenga uhusiano wa karibu na kuboresha ushirikiano katika sekta ya nishati. Ziara hiyo imefanyika katika Ofisi za TPDC zilizopo Jengo la Benjamin Mkapa- Posta Jijini Dar es Salaam. Ziara hiyo ilijikita katika kuelewa zaidi namna Shirika linavyofanya kazi na changamoto…

Read more →
26
Mar

NAIBU WAZIRI MKUU NA WAZIRI WA NISHATI AZINDUA RASMI KIWANDA CHA UWEKAJI MIFUMO MBALIMBALI KWENYE MABOMBA YA MRADI EACOP

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto Biteko amefanya uzinduzi rasmi wa Kiwanda cha uwekaji mifumo mbalimbali katika mabomba yatakayotumika kusafirisha mafuta ghafi mradi wa EACOP kutoka Hoima nchini Uganda hadi Tanga Tanzania tarehe 26.03.2024. Dkt. Biteko amesema kwamba ujenzi wa Mradi huo unaendelea vizuri ambapo hadi sasa kwa upande wa eneo la kuhifadhia mafuta ujenzi wa matenki makubwa manne Chongoleani Tanga umefikia asilimia 37 huku ujenzi…

Read more →
1 2 3 7