Our Latest Blog Posts
27
Jun

SERIKALI YAONDOA TOZO KWENYE GESI ASILIA

Serikali imeridhia ombi la kuondoa ushuru wa shilingi 382 iliyokuwa imepanga kuweka kwenye kila kilo ya gesi asilia inayotumika kwenye magari kuanzia mwaka ujao wa fedha 2024/25. Ushuru huo umeondolewa kufuatia ushauri wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti ambayo imeeleza kuwa haikubaliani na ushuru huo kwani sekta ya gesi bado ni changa na inaendelea kukua taratibu na hadi sasa haijaweza kutumika kikamilifu nchini kutokana na gharama za kufunga…

Read more →
13
Jun

WAJUMBE WA BODI YA WAKURUGENZI TPDC, WATEMBELEA MIRADI YA UWAJIBIKAJI KWA JAMII (CSR)

Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) limeendelea kuunga mkono juhudi za Serikali katika kuboresha huduma za kijamii kwenye maeneo ambayo shughuli za utafutaji, uzalishaji, usafirishaji na usambazaji wa gesi asilia zinafanyika. Huduma hizo ni pamoja na afya, elimu, maji na utawala bora ambapo huduma hizi ni sehemu ya Uwajibikaji wa Shirika kwa Jamii (CSR). Hayo yamebainishwa katika ziara ya Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya TPDC walipotembelea miradi mbalimbali…

Read more →
12
Jun

TPDC YAPONGEZWA KUENDESHA VIWANDA VYA KUCHAKATA GESI KWA KUTUMIA WAZAWA

Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi TPDC wamepongeza jitihadaa zinazofanywa na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) katika kuwajengea uwezo wafanyakazi wanaoendesha mitambo ya kuchakata gesi asilia Songosongo na Madimba ikiwa ni pamoja na kutoa mafunzo ya muda na muda mrefu ndani na nje ya nchi. Mkakati huu imewezesha wafanyakazi hao kuwa na uwezo mkubwa wa kuendesha mitambo hiyo kwa ufanisi wa hali ya juu. Akiongea baada ya ziara hiyo, Mjumbe…

Read more →
07
Jun

TPDC YAWEKA MKAKATI WA KUWA NA HIFADHI KUBWA YA MAFUTA NCHINI

Hayo yameelezwa katika ziara ya Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) inayoongozwa na Mhe. Balozi Ombeni Sefue wakati wa ziara ya kutembelea miradi ya TPDC iliyopo TIPER Kigamboni leo tarehe 07/6/2024. Lengo la ziara hiyo ni kujionea hali halisi ya miundombonu ya miradi ambayo kwa muda mrefu imekua haitumiki pamoja na kueleza mikakati iliyopo ya ukarabati na ujenzi wa miundimbinu mingine mipya ili nchi iwe…

Read more →
17
May

TPDC, ROSETTA NA AFRICA 50 ZASAINI MKATABA WA UBIA WA KUSAMBAZA GESI ASILIA NCHINI

Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) na Kampuni ya Rosetta ya nchini Misri wamesaini mkataba wa awali wa ubia wa utekelezaji wa mradi wa kusambaza gesi asilia kwa mfumo wa Mini LNG. Mkataba huo umesainiwa leo tarehe 17/05/2024 katika ukumbi wa mikutano wa TPDC ulioko Jengo la Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam. Akizungumza katika hafla hiyo kwa niaba ya Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mkurugenzi Mkuu…

Read more →
02
Apr

NAIBU KATIBU MKUU WIZARA YA NISHATI AFANYA ZIARA TPDC

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Dkt. James Mataragio,amefanya ziara ya kikazi katika  Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) na kuzungumza na Menejimenti ya TPDC  lengo likiwa ni kujenga uhusiano wa karibu na kuboresha ushirikiano katika sekta ya nishati. Ziara hiyo imefanyika katika Ofisi za TPDC zilizopo Jengo la Benjamin Mkapa- Posta Jijini Dar es Salaam. Ziara hiyo ilijikita katika kuelewa zaidi namna Shirika linavyofanya kazi na changamoto…

Read more →
26
Mar

NAIBU WAZIRI MKUU NA WAZIRI WA NISHATI AZINDUA RASMI KIWANDA CHA UWEKAJI MIFUMO MBALIMBALI KWENYE MABOMBA YA MRADI EACOP

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto Biteko amefanya uzinduzi rasmi wa Kiwanda cha uwekaji mifumo mbalimbali katika mabomba yatakayotumika kusafirisha mafuta ghafi mradi wa EACOP kutoka Hoima nchini Uganda hadi Tanga Tanzania tarehe 26.03.2024. Dkt. Biteko amesema kwamba ujenzi wa Mradi huo unaendelea vizuri ambapo hadi sasa kwa upande wa eneo la kuhifadhia mafuta ujenzi wa matenki makubwa manne Chongoleani Tanga umefikia asilimia 37 huku ujenzi…

Read more →
23
Mar

PIC YAFURAHISHWA NA UWEKEZAJI WA SERIKALI KATIKA SEKTA YA MAFUTA NA GESI

Kamati ya kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) imefurahishwa na matokeo ya uwekezaji uliofanywa na Serikali katika Sekta ya mafuta na gesi asilia nchini. Hayo yamejiri wakati wa ziara maalumu ya Kamati hiyo ilipotembelea mitambo ya uchakataji gesi asilia ya Mnazi bay na Madimba Mkoani Mtwara. Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Deus Sangu (Mb) alisema kuwa Kamati imefurahishwa na matokeo ya uwekezaji uliofanywa na unaoendelea kufaywa…

Read more →
20
Mar

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA HESABU ZA SERIKALI (PAC) YARIDHISHWA NA MATUMIZI YA FEDHA ZINAZOTOLEWA NA SERIKALI MRADI WA EACOP

Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Hesabu za Serikali (PAC) imefanya ziara ya kikazi katika Kiwanda cha kuweka mifumo ya kupasha joto mabomba ya mradi wa bomba la kusafirisha mafuta ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) kilichopo eneo la Sojo Wilaya ya Nzega Mkoani Tabora. Akizungumza katika Ziara hiyo, Makamu Mwenyekiti wa Kamati Mhe. Japhet Hasunga (Mb) alisema kuwa ziara ya kamati hiyo ililenga kuangalia mambo matatu ambayo ni; kuangalia uwekezaji…

Read more →
31
Aug

KAMPUNI TANZU ZA TPDC; GASCO NA TANOIL ZAPATA BODI ZA KUDUMU

Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) leo tarehe 31/08/2023 limezikabidhi rasmi Kampuni zake Tanzu za GASCO na TANOIL miongozo na Sheria mbalimbali zitakazowaongoza katika utekelezaji wa majumu yao mapya. Aidha, Mwenyekiti wa Bodi ya TPDC, Balozi Ombeni Sefue amewaasa Wenyeviti na Wajumbe wa Bodi hizo kutafsiri malengo ya Shirika mama (TPDC) yaliyotolewa na Serikali na kuhakikisha Menejimenti za Kampuni hizo zinatekeleza Majukumu yao kwa ufanisi na kuleta faida katika…

Read more →